Bomoa bomoa Mwenge yawaliza wengi Dar
Tingatinga likiwa kazini kubomoa nyumba zilizo ndani ya hifadhi ya barabara.
Vumbi likiwa limetanda eneo hilo.
Ulinzi ukiwa umeimarishwa eneo la tukio.
Baadhi ya wakazi wa eneo hilo wakiwa wameduwaa baada ya kubomolewa nyumba zao.
Baadhi ya wafanyabiashara wakiokota baadhi ya vitu vyao vilivyovunjika wakati wa zoezi.
….Wakiendelea kuokota baadhi ya vitu.
… Wakionekana kushauriana jambo.
Friji zilizovunjika wakati wa bomoabomoa.
Wahanga wa tukio wakijadiliana.
Mhanga wa ubomoaji akiokotoza kilichobakia.
Muonekano wa baadhi ya vyombo vikiwa barabarani baada ya bomoabomoa.
Huzuni ikiwa imetanda kwa baadhi ya vijana waliobomolewa nyumba zao.
Hali halisi ilivyokuwa kufuatia ubomoaji huo.
NYUMBA zilizopo katika Manispaa ya Wilaya ya Kinondoni Jijini Dar es Salaam maeneo ya (TRA) Mwenge kupitia barabara ya Afrika Sana zimebomolewa na tingatinga kwa madai ya kuwa eneo hilo ni hifadhi ya barabara na tayari manispaa ilikuwa imekwisha kutoa taarifa (notice) ya kuondoa eneo hilo.
Kamera yetu imenasa matukio yanayoonesha tingatinga likibomoa nyumba hizo huku baadhi ya vitu vya wamiliki wa nyumba hizo vikionekana kuvunjika.
(Na Denis Mtima./GPL)

