Bomoabomoa Dar, Herieth aangua kilio
Stori: Imelda Mtema
Machozi! Mwigizaji mkongwe wa Bongo Movies, Herieth Chumila amejikuta akiangua kilio baada ya nyumba yake kukumbwa na bomoabomoa wakati wowote kutoka sasa.
Herieth aliliambia gazeti hili kuwa, hakuna kinachomuuma kama kubomolewa nyumba ambayo alijibana kwa muda mrefu hadi akaijenga na kukamilika hivyo kubomolewa kwake itamuweka kwenye wakati mgumu na maumivu makubwa.