Bonga Aachana na Harmonize, Atimkia Lykos Empire – Video
Prodyuza wa Harmonize almaarufu kwa jina la Bonga leo ametangaza rasmi kuachana na msanii huyo na kujiunga lebo ya Lykos Empire ambapo ataendelea kuwa prodyuza na muimbaji.
Akizungumza na wanahabari kwenye mkutano uliofanyika Hoteli ya King D, leo mchana Bonga amesema sababu kubwa iliyomuahamisha ni kutafuta maslahi ya kimaisha.
Akijibu maswali ya wanahabari Bonga alikanusha kuondoka kwa Harmonize baada ya kutofautiana nae na kusistiza kuwa lengo kubwa la kuhama ni kupanua mawazo na kusaka maslahi zaidi.
HABARI:NEEMA ADRIAN PICHA: RICHARD BUKOS/GPL