The House of Favourite Newspapers

Boniface Jacob Ashinda Uchaguzi wa Meya Manispaa Ubungo

1

Diwani wa Kata ya Ubungo ambaye pia alikuwa Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni kabla madiwani wake hawajagawanyika, Boniface Jacob (pichani) ameshinda katika uchaguzi wa Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo uliofanyika mapema leo mchana.

Mhe. Boniface Jacob kupitia Chadema ambaye pia anaungwa mkono na UKAWA ameshinda kwa kura 16 kati ya kura 18 za wajumbe.

jacob

Matokeo hayo yametangazwa na katibu wa mkutano huo DED Kayombo na yalikuwa kama ifuatavyo;

Nafasi ya Naibu Meya wapiga kura walikuwa 18, Kura halali zilikuwa 18, kura zilizoharibika 0.

Abdul Lema wa CCM amepata kura 3, Kwangaya Ramadhani wa Ukawa amepata kura 15 hivyo Kwangaya Ramadhani (Ukawa) ndiye Naibu Meya wa almashauri ya Manispaa ya Ubungo.

Nafasi ya Meya Wapiga kura walikuwa 18, Kura zote halali zilikuwa 18, Kura zilizoharibika ni 0.

Yenga CCM alipata kura 2 huku Boniface Jacob akipata kura 16.

Kwa matokeo hayo, Mhe. Boniface Jacob ndiye Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo.

Comments are closed.