The House of Favourite Newspapers

Bosi Azam Akiri Mambo Magumu

0
Ofisa Mtendaji Mkuu wa Azam FC, Abdulkarim Amin ‘Popat’.

HATIMAYEuongozi wa Azam FC, umekiri kuwa katika wakati mgumu kutokana na timu hiyo kukosa matokeo mazuri katika michezo sita iliyopita ya ligi huku wakishindwa kujua sababu ya matokeo hayo mabovu.

 

Azam FC ambayo hapo awali iliongoza ligi, imejikuta katika mfululizo wa matokeo mabovu ambapo katika michezo sita ya mwisho imetoa sare nne na kupoteza mbili.

Aki-zungumza na Spoti Xtra, Ofisa Mtendaji Mkuu wa Azam FC, Abdulkarim Amin ‘Popat’ alisema: “Sijui kwa nini timu haipati ushindi, kila kitua ambacho kinatakiwa kupatikana ndani ya Azam kinapatikana.

“Wachezaji wote wanapata stahiki zao mapema na kwa wakati, labda utakuwa ni upepo tu mchafu ndio umetupitia, lakini hatujakata tamaa, tutaendelea kupambana ili mambo yaendelee kuwa mazuri.

Leave A Reply