Break Up Day iliniumiza sana kichwa – Sarah Kim
Stori: Ng’osha Gabriel
Mwanamuziki wa Muziki wa Hip Hop, Sarah Hopah Kimario ‘Sarah Kim’ ameibuka na kusema kwamba ngoma yake mpya ya Break Up Day ndiyo iliyomuumiza kichwa chake katika kipindi alichokuwa akiitunga.
“Nilipata wakati mgumu sana,” alisema Sarah na kuongezea:
“Sikuamini kama ningeweza kuandika wimbo mkali kama huu. Nilipata wakati mgumu sana, niliandika mistari, nikafuta, yaani kila idea iliyokuja kichwani niliiona kutokufaa ila mwisho wa siku, nikatunga wimbo huu” alisema Sarah.
Sarah ni msomi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam mwaka wa pili anayechukua kozi ya Computer Engineering. Kwa sasa, ngoma zake zote anazifanyia katika Studio ya Tunes Production chini ya Prodyuza Eddy Lesser.