The House of Favourite Newspapers

BREAKING: JPM Amteua Diwani Kuwa Mkurugenzi Mkuu Usalama

Rais  John  Magufuli akimuapisha Kamishna Diwani Athuman Msuya kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Usalama wa Taifa Ikulu Jijini Dar es Salaam, ambaye anachukua nafasi ya Dkt. Modestus Kipilimba.

RAIS  wa Tanzania, John Magufuli, amemteua na kumuapisha Diwani Athuman kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Usalama wa Taifa kuchukua nafasi ya Dk Modestus Kipilimba.

…Akimkabidhi vitendea kazi Kamishna  Msuya.

Taarifa iliyotolewa leo Alhamisi Septemba 12, 2019 na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu, Gerson Msigwa inaeleza kuwa uteuzi wake umeanza leo.

…Akizungumza mara baada ya kumuapisha.

Kabla ya uteuzi huo, Diwani aliyeapishwa Ikulu, Dar es Salaam leo alikuwa Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru).

…Akisaini hati ya kiapo baada ya kumwapisha Kamishna Diwani.

Akizungumza baada ya kumwapisha, Rais Magufuli amemtaka kuchapa kazi kwa juhudi na maarifa na kuweka mbele maslahi ya taifa.

Taarifa hiyo inaeleza kuwa Kapilimba atapangiwa kazi nyingine.

Athumani aliteuliwa kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Takukuru  Septemba 6, 2018, nafasi aliyoitumikia kwa mwaka mmoja na siku sita. Kabla ya kwenda Takukuru alikuwa Katibu Tawala wa Mkoa (RAS) Kagera.

Nafasi alizoshika Kamishna Diwani Msuya tangu 2015:

⭕️2015: Kaimu Kamishna wa Kamisheni ya Intelijensia ya Jinai
⭕️Mei 2015: Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI)
⭕️Nov. 2016: Katibu Tawala Kagera
⭕️Sep. 2018: Mkurugenzi Mkuu TAKUKURU
⭕️Sep. 2019: Mkurugenzi Mkuu TISS

Picha na Ikulu

Comments are closed.