The House of Favourite Newspapers

BREAKING NEWS: Majambazi Wanne Wauawa na Polisi Kariakoo (Pichaz)

0

DAR ES SALAAM: Jeshi la Polisi limewaua watu wanne wanaodhaniwa kuwa ni majambazi wakati wakivamia maduka Kariakoo, Mtaa wa Aggrey / Livingstone usiku wa kuamkia leo.

Mashuhuda wa tukio hilo wameeleza kuwa majibizano ya risasi kati ya polisi na majambazi yalichukua takribani dakika 10 huku majambazi hao wakionekana kuzidiwa na kuuawa kwa kupigwa risasi na polisi hao.

Imeelezwa kuwa, kutokana na purukushani hizo za majibizano ya risasi kati ya majambazi na jeshi la polisi, baadhi ya watu waliokuwa eneo la tukio wamejeruhiwa kwa risasi ambapo mmoja wao amepelekwa hospitali.

Taarifa zaidi tutawajuza kadri tutakavyozipata.

 

Leave A Reply