Mchakato wa Sheria ya Vyama vya Siasa Kuanza Hivi Karibuni
BARAZA la Vyama vya Siasa limesitisha mjadala wa mapendekezo ya marekebisho ya sheria mpya ya vyama vya siasa na kurudisha mchakato huo katika kamati ya sheria na utawala bora, kamati ya uongozi ya baraza hilo.
Sasa kamati hizo zinatakiwa kujadili marekebisho ya kanuni za usajili wa vyama vya siasa baada ya baraza hilo kushindwa kujadili.
Akizungumza leo Januari 18, 2018 mwenyekiti wa baraza hilo, John Shibuda amesema mapendekezo hayo yanatakiwa kukamilika baada ya mwezi mmoja kabla ya kuitisha baraza maalum litakalopitia suala lililopaswa kufanywa leo.
Kikao hicho kilihudhuriwa na wajumbe 38, akiwemo Naibu Katibu Mkuu wa Chadema Zanzibar, Salum Mwalimu, Makamu Mwenyekiti wa CCM Bara, Philip Mangula na Naibu Katibu Mkuu wa chama hicho Zanzibar, Dk Abdallah Juma Saadala.
PICHA NA DENIS MTIMA | GPL
FUATILIA VIDEO YA TUKIO HILO
Comments are closed.