Breaking News: Adhabu Ya Mwakalebela Yatenguliwa na TFF
MAKAMU Mwenyekiti wa klabu ya Yanga Fedrick Mwakalebela leo Juni 24, 2021 ameshinda kesi ya maombi ya marejeo mbele ya kamati ya maadili ya TFF dhidi ya hukumu ya kufungiwa miaka mitano kujishughulisha na mpira wa miguu ndani na nje.
Kamati hiyo iliyoketi Juni 23, imeridhia kumuondolea adhabu ya kifungo cha miaka mitano Pamoja na faini ya jumla ya sh. milioni saba.
Mwakalebela katika katika maombi yake amesema anajutia kosa hivyo anaomba aondolewe adhabu hiyo amabyo ameitii kwa kipindi chote, aliomba apewe fursa nyingine ya kutumikia mpira wa miguu.