KLABU ya Everton ya Uingereza tayari imewasili katika ardhi ya Tanzania tayari kwa mchezo wa kirafiki wa kesho dhidi ya Gor Mahia ya nchini Kenya, mchezo utakaopigwa katika Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.
Wakali hao wamewasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam mapema leo asubuhi na kupokelewa na uongozi wa wadhamini wao, SportPesa ambao ndio wamewaleta hapa nchini.
Baada ya kuwasili walielekea hotelini kwa ajili ya mapumziko kisha baadaye watapata fursa ya kufanya mazoezi.
Hiki hapa kikosi kamili cha Everton waliowasili Tanzania leo:
Maarten Stekelenburg, Mateusz Hewelt, Chris Renshaw, Tom Davies, Phil Jagielka, Ashley Williams, Callum Connolly, Jonjoe Kenny, Michael Keane, Muhamed Besic, Leighton Baines, Morgan Schneiderlin, James McCarthy, Davy Klaassen, Gareth Barry, Idrissa Gana Gueye, Joe Williams, Kieran Dowell, Kevin Mirallas, Wayne Rooney, Aaron Lennon, Dominic Calvert-Lewin, Ademola Lookman, Matthew Pennington, Yannick Bolasie.
Everton walivyoondoka Uingereza
| The Everton squad has departed for Tanzania with @WayneRooney part of the squad. #EvertonInTz
Full list https://t.co/d91hPajhey pic.twitter.com/AS8Lt3Xz51
— Everton (@Everton) July 11, 2017