BREAKING: LORI LA MAFUTA LATEKETEA KWA MOTO MBEYA – VIDEO
ROLI lililokuwa limebeba shehena ya mafuta ya petroli likitokea jijini Dar-es-Salaam kuelekea nchini Malawi limeteketea kwa moto leo katika eneo la Stamiko wilayani Rungwe mkoani Mbeya.
Jitihada za kuzima moto huo zinafanywa na kikozi cha zima mato na uokoaji kwa kushirikiana na jeshi la polisi na wananchi huku chanzo cha moto huo kikiwa bado hakijajulikana.
Mpaka sasa hakuna mamlaka yoyote ambayo imezungumzia tukio hilo, pia hakuna kifo wala majeruhi aliyeripotiwa kutokana na tukio hilo.
GLOBAL TV – RIPOTA ni You Tube Channel ya Jamii, inakupa nafasi wewe mdau ku share habari na matukio ya kipekee na wenzio popote walipo duniani, kwa kutumia simu yako ya mkononi. Popote ulipo unapokutana na tukio ambalo unaweza kulinasa kwa njia ya video ya simu yako, basi usisite kufanya hivyo na kisha tutimie kwenda namba 0753 715 779 (+255753715779) tutakulipa mkwanja chapchap.
Comments are closed.