The House of Favourite Newspapers

Waziri, Mkuu Majaliwa ashinda kwa asilimia 73.5

majaliwaWaziri Mkuu Mteule Mhe. Majaliwa Kassim Majaliwa.
e016df6a-9405-4fcb-8a4c-a6cc56bfa773Mpambe wa Rais Kanali Mkeremi akiingia bungeni mjini Dodoma leo asubuhi akiwa na bahasha yenye jina la Waziri Mkuu mteule lililowasilishwa  na  Rais Dkt. John Pombe Joseph Magufuli ili kupigiwa kura na hatimaye kuridhiwa na wabunge.Majaliwa kassim (1)Spika Job Ndugai akiinua bahasha kabla ya kusoma  jina la Waziri Mkuu mteule lililowasilishwa bungeni  na  Rais Dkt. John Pombe Joseph Magufuli ili kupigiwa kura na hatimaye kuridhiwa na wabunge.Majaliwa kassim (2)Wakati hayo yakiendelea ndani ya bunge Mbunge wa Rwangwa Mhe. Majaliwa Kassim Majaliwa akiwasili viwanja vya bunge akiwa peke yake bila shaka akiwa hana habari kwani usiri wa kupatikana na hatimaye kuwasilishwa jina la Waziri Mkuu Mteule ulikuwa mkubwa sana.
Majaliwa kassim (3)Bunge linaripuka na wabunge wanampongeza Waziri Mkuu Mteule Mhe. Majaliwa Kassim Majaliwa baada ya jina lake kutangazwa na hatimaye kupigiwa kura na kupita kwa kishindo kwa kura 258 ama asilimia 73.5 ya idadi ya kura zilizopigwa.
Majaliwa kassim (5)Bunge linaripuka na wabunge wanampongeza Waziri Mkuu Mteule Mhe. Majaliwa Kassim Majaliwa baada ya jina lake kutangazwa.
Majaliwa kassim (4)Waziri Mkuu Mteule Mhe. Majaliwa Kassim Majaliwa akimtanguliza  Mwenyezi Mungu kwa kumjaalia nafasi hiyo, akimshukuru Rais Dkt. John Pombe Joseph Magufuli kwa imani aliyoonesha juu yake, anawashukuru pia wabunge kwa kumpa kura nyingi, na wapiga kura wake kwa kumchagua tena na kumuwezesha kufika hapo. Picha na Sultani Kipingo.

Waziri Mkuu Mteule wa Awamu ya Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Majaliwa Kassim Majaliwa ameshinda kwa kura za ndiyo 258 sawa na asilimia 73.5 ya kura zote zilizopigwa na wabunge leo, wakati kura za hapana zikiwa 91, sawa na asilimia 25.9.

Kassim Majaliwa alizaliwa Desemba 22, 1960 na ana umri wa miaka 54.

Ni Mbunge wa Jimbo la Ruangwa mkoani Lindi kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) na alikuwa Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi).

WASIFU WAKE:

Elimu
Toka Hadi Jina la Shule/Chuo Cheti
1970 1976 Mnacho Primary School Cheti cha Elimu ya Msingi
1977 1980 Kigonsera Secondary School CSEE
1991 1993 Mtwara Teachers College
1994 1998 University of Dar es Salaam Bachelor Degree
1999 1999 Storckolm University PGDP
Uzoefu
Toka Hadi Jina la Mwajiri Ngazi/Wazifa
2010 2014 MB
2006 2010 PM Mkuu wa Wilaya
2001 2006 PS-CWJ Katibu Mkoa
2001 2001 PS-CWJ Katibu Wilaya
1988 2000 PS-Moec Mkufunzi
1984 1986 TD-Lindi Council Mwalimu
Burudani
  •   Soka

Comments are closed.