Breaking News: Mbunge Mwigulu Nchemba Apata Ajali Mbaya
Taarifa zilizothibitishwa na Jeshi la Polisi zimeeleza kuwa, Mbunge wa Iramba Magharibi (CCM), Dkt. Dk Mwigulu Lameck Nchemba amepata ajali ya gari leo Jumatano, Februari 13, 2019 asubuhi akiwa njiani katika Barabara ya Iringa kuelekea Dodoma.
Imeelezwa kuwa, chanzo cha ajali hiyo ni gari lake liligonga Punda barabarani ambapo baada ya ajali hiyo, amekimbizwa katika Hospitali ya Dodoma kwa ajili ya matibabu zaidi.
Comments are closed.