The House of Favourite Newspapers

CHIRWA RUKSA LIGI KUU, MSUVA APEWA ONYO

0
Msuva akimfuata mwamuzi.

MSHAMBULIAJI wa Yanga, Obrey Chirwa na kiungo wa Singida United, Deus Kaseke wameruhusiwa kucheza mechi za Ligi Kuu Bara kufuatia kutokutwa na hatia katika tuhuma iliyokuwa ikiwakabili ya kumwangusha mwamuzi Charles Ludovic katika msimu uliopita dhidi ya Mbao FC.

Kamati ya Nidhamu ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) ambayo imepitia shauri hilo imemkuta na hatia aliyekuwa kiungo mshambuliaji wa Yanga, Simon Msuva ambaye kwa sasa anacheza katika Klabu ya Diffa Al Jadida ya Morocco baada ya ushahidi kuonyesha kuwa ndiye aliyemsukuma mwamuzi hivyo kupewa onyo kali.

Mshambuliaji wa Yanga, Obrey Chirwa.

Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Nidhamu ya TFF, Peter Hellar amesema kamati yake haikuwakuta na hatia wachezaji Chirwa na Kaseke katika shitaka hilo kupitia ushahidi mbalimbali walioutazama na badala yake Msuva ndiye aliyekutwa na kosa ambapo kwa mujibu wa sheria alitakiwa kukosa mechi tatu lakini kwa sasa amepewa onyo.

“Kamati ilitoa nafasi kwa walalamikiwa na walalamikaji kutoa ushahidi ambapo ushahidi mwingine uliotumika ni video na kamati na ripoti ya kamisaa na mwamuzi na kwa baadhi ya wachezaji aliyekuwa ni Chirwa na Kaseke lakini Msuva hakuwepo kutokana na kutokuwepo nchini.

“Kamati ilipopitia shauri hilo ilimkuta Msuva ndiye mwenye hatia ambapo alionekana akimwangusha mwamuzi, hivyo anatiwa hatiani kwa ibara ya (49) (1) B ambapo chini ya kifungu hiki anatakiwa kukosa si chini ya mechi tatu, lakini kwa upande wa wachezaji waliobakia kamati haikuwakuta na hatia.

“Hata hivyo kamati ya ligi ilitoa adhabu kabla ya kamati ya nidhamu kinyume na taratibu hivyo ni vyema TFF kupitia kamati zake ikafanya maamuzi haraka mara baada ya tukio kutokea ili kuepuka jambo kama hili,” alisema Peter.

Aidha, Ofisa Habari wa TFF, Alfred Lucas alisema Msuva aliwasili nchini jana baada ya kufanikiwa kupata viza, tayari ameshajiunga na wenzake wa Taifa Stars kuivaa Botswana.

Stori: Khadija Mngwai | Championi Ijumaa

Global Publishers App

TAZAMA VIDEO YA TUKIO HILI

Usipitwe na Matukio, Install ===>Global Publishers App

Sikiliza Hadithi za Mtunzi Eric Shigongo Hapa

Mawakili Kanda ya Ziwa Waliamsha Dude kwa Lissu

 

Leave A Reply