The House of Favourite Newspapers

VIDEO: #GlobalBreakingNews: Sakata la Makinikia… Chadema Wafunguka LIVE

0

DAR: Uongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) umeibuka na kuzungumzia sakata la mchanga wa madini (makinikia) ambalo kwa sasa ndilo linachukua headlines kwenye vyombo mbalimbali vya habari.

Akizungunmza na wanahabari Katibu Mkuu wa Chadema Taifa, Dkt. Vicent Mashinji ameseeleza namna ambavyo chama chao kimekuwa mstari wa mbele kukemea mikataba mibovu ya madini jambo ambalo lilipelekea aliyekuwa mbunge wao, Zitto Kabwe kusimamishwa kuhudhuria bunge mwaka 2017.

Pamoja na hayo, Dkt. Mashinji amekemea kitendo cha wabunge wa chama chake, Ester Bulaya na Halima Mdee kusimamishwa Bunge hadi mwakani kitendo ambacho amesema kinawanyima fursa wabunge hao kuwawakilisha wananchi wao bungeni.

Katika masuala ya saikolojia (medical psychology) mtu hawezi kupewa mapendekezo zaidi ya 20 halafu akayakubali yote kwa asilimia 100 bila kuwa na chembe ya wasiwasi. Rais aliyakubali mapendekezo yote ya kamati kwa sababu ripoti ile ya uchunguzi wa mchanga wa madini aliiandika yeye mwenyewe, alieleza kiongozi wa CHADEMA.

“Kisaikolojia haiwezekani kitu ambacho hukijui ukakikubali chote bila kuwa na mashaka,” alisema Katibu Mkuu wa Chama cha Demikrasi na Maendeleo (CHADEMA), Dkt. Vicent Mashinji.

Kiongozi huyo ametoa kauli hiyo leo alipokuwa  akizungumza na waandishi wa habari kuelezea msimamo wao juu ya sakata la madini ambapo wamesema wao hawawezi kushangilia maneno matupu bali wanasubiria matokeo.

“Tunataka kuona hatua kwanza na sio pongezi ambazo sasa hivi zinaambatana na ushabiki wa kisiasa na kauli tupu nyingi nyingi, mara mwizi, mara mwanaume.”

Aidha, Dkt Mashinji alimtaka Rais Magufuli kuueleza umma wa Watanzania kama kampuni ya Barrick ambao ni wamiliki wakubwa wa Acacia ni wezi au ni wanaume. Akitolea ufafanuzi, neno mwanaume, Dkt Mashinji alisema kwa mazingira ya kitanzania neno mwanaume linamaanisha mtu mchapakazi, mtenda haki, anayejituma. Hivyo Rais aseme kama Barrick ni wezi au wachapakazi.

“Ukiongea katika lugha ya kitanzania ukisema huyu jamaa ni mwanaume kwelikweli, tafsiri yake ni rahisi tu, kwamba huyu jamaa ni mchapakazi, ni muungwana ni mtu wa watu, ndivyo tunavyotumia. Hatuongelei mwanaume kwa sababu ya maumbile yake.“

Wakati huo huo, Dkt Mashinji alisema, kama Rais Dkt Magufuli anawapenda Watanzania kama ambavyo anadai, awape katiba ya Warioba kwani ndiyo chaguo lao na ndio itakayomaliza matatizo yote.

Alisema kuwa, wao waamini kama Rais ataruhusu mchakato wa katiba ya Warioba kupitishwa, basi wabunge wa CCM wanaopitisha sheria kiushabiki na kutotimiza majukumu yao hawatarudi bungeni sababu watawajibishwa na wananchi.

Leave A Reply