The House of Favourite Newspapers

Spika Tulia Awakingia Kifua Wabunge 19 waliovuliwa Uanachama na CHADEMA

0
Spika wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt, Tulia Akson

SPIKA wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Tulia Ackson amewakingia kifua wabunge 19 wa kuteuliwa kutoka Chama Cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA ambao walivuliwa uanachama na Chama hicho Mei 12 Jijini Dar es Salaam.

 

Akiongea Bungeni katika Bunge la 12 la Bajeti, Mkutano wa 7 kikao cha 23 amebainisha kama Spika kupokea barua kutoka kwa Katibu Mkuu wa CHADEMA John Mnyika ikimtaarifu juu ya maamuzi ya Kamati Kuu ya Chama hicho kuhusu kuwavua uanachama Wabunge 19 kutoka chama hicho.

Spika Tulia amesema Bunge haliwezi kuingilia jambo ambalo lipo Mahakamani na Kwa mujibu wa Katiba ya nchi Mamlaka yenye kauli ya mwisho kwenye utoaji hai ni Mahakama, hivyo maamuzi ya Mahakama ndiyo yatakayotoa hatima ya Wabunge hao.

Wabunge 19 wa CHADEMA waliovuliwa Uanachama

Spika Tulia amesisitiza kuwa maswali yeyote kuhusu jambo hilo mtu rasmi wa kuyajibia hayo dani ya Bunge ni Spika wa Bunge na si mtu mwingine yeyote.

Leave A Reply