Breaking: Rais Samia Ampendekeza Dkt. Mpango Kuwa Makamu wa Rais
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na na Amiri Jeshi Mkuu, Mhe. Samia Suluhu Hassan amempendekeza Dkt. Phillip Mpango kuwa Makamu wake wa Rais. Mpambe wa Rais (ADC) amewasilisha jina hilo kwa Spika wa Bunge, Job Ndugai, Bungeni, Dodoma leo Machi 30, 2021 kwa ajili ya kuthibitishwa na Bunge.