The House of Favourite Newspapers

Breaking: Watoto 6 Wafariki kwa Radi, 25 Wajeruhiwa Geita

TAARIFA zilizotufikia hivi punde zinaeleza wanafunzi sita wa Shule ya Msingi ya Emaco Vision English Medium ya mjini Geita wamefariki dunia leo na wanafunzi wengine 25 wamejeruhiwa baada ya kupigwa na radi wakiwa darasani.

Ofisa Elimu Msingi wilayani Geita, Yese Kanyuma, amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kusema mvua kubwa iliyoambatana na radi imenyesha leo asubuhi na kusababisha madhara hayo.

 

“Tukio hilo la radi limetokea majira ya saa 3 asubuhi na kusababisha vifo vya wanafunzi sita wa darasa la pili na la tatu, wengine 25 wamejeruhiwa lakini wanaendelea na matibabu wodini. Tunawashukuru madaktari na wauguzi kwa jitihada zao kuokoa maisha ya watoto hao waliojeruhiwa,” amesema Kanyuma.

Comments are closed.