The House of Favourite Newspapers

Buku ya Sokabet Yampa Milioni 2 Fundi Magari

0
Frank Chodaus.

MKAZI wa Mikumi mkoani Morogoro, Frank Chodaus amekuwa ni mmoja wa wanaonufaika na mchezo wa kubashiri matokeo kutoka kampuni ya Sokabet baada ya kujishindia shilingi milioni 2 baada ya kubashiri kwa kutumia shilingi 1000 tu.

Ndani ya tovuti ya kampuni hiyo ya Sokabet kila wiki huwa kuna kipengele kinachowawezesha washiriki kushinda hadi shilingi milioni 100 kwa kubashiri matokeo kwa shilingi elfu moja tu, ambapo ndipo huko Frank aliponufaika.

Akizungumza juu ya ushindi huo mratibu wa Kampuni ya Sokabet, Franko Ruhinda alisema mshindi huyo alipatikana wikiendi iliyopita baada ya kupatia michezo 11 kati ya 13 ambayo alitakiwa kupatia kwenye kipengele hizo cha Jackpot.

“Unajua kama ambavyo tumekuwa tukishauri watu kuendelea kujiunga na kushiriki katika Sokabet, ndani ya muda mfupi wanaweza kujiingizia mamilioni kwa kuweka fedha kidogo tu katika ubashiri wao, ushindi wa Frank ni mfano tu wengi wanaojishindia ndani ya tovuti yetu,” alisema Franko.

Alipowasiliana na mwandishi wa habari hii, mshindi huyo alisema ilikuwa ni furaha kwake kupata fedha hizo kwa kuwa hakutegemea lakini ni jambo muhimu kwa kuwa fedha hizo zimemwezesha kutatua matatizo yake mengi.

Akifafanua zaidi alisema: “Mimi ni fundi magari na nimekuwa nikishiriki sana katika michezo hii ya kubet, sasa Sokabet ilivyoanzishwa kwanza sikujiunga kwa kuwa nilikuwa sijapata elimu vizuri, baada ya kufatilia magazeti ndipo nikawajua vizuri na kujiandikisha.

“Nilipojiandikisha nikaanza kubet mdogomdogo, mwanzoni sikupata, lakini kila wiki nimekuwa nikibet katika vipengele tofauti kikiwemo kipengele cha Jackpot.

“Sasa wiki iliyopita, nilibet kama kawaida kwa buku (Sh 1,000), baada ya hapo nikaendelea na shughuli zangu, sikufuatilia majibu kwa kuwa mechi nyingi ziliisha usiku wa Jumamosi.

“Kawaida huwa nikibet kama hivyo nasubiri kuona kama nitapata ujumbe, nikiona sijapata dnipo nafungua akaunti yangu ya kubet na kuangalia nilipokosea,

“Sasa Jumapili nikashtukia nikipata ujumbe kuwa nimeshinda shilingi milioni 2, ilikuwa furaha kubwa kwangu kwa kuwa sikutegemea na unajua wakati mwingine hivi vitu ni bahati.”

Aliongeza kwa kusema haya: “Hicho kipengele mtu anatakiwa kupatia michezo 13 ambapo kama ningefanikiwa hivyo maana yake ningepata milioni mia, na kama ningepatia michezo 12 ningepata milioni tano, ila mimi nilipatia michezo 11.”

Kuhusu matumizi ya fedha hizo, fundi huyo ambaye ana umri wa miaka 25 alisema zilimsaidia katika matumizi yake lakini ataendelea kubet kwa kuwa anaamini anayo nafasi nyingine ya kupata mzigo mkubwa zaidi ya alioupata mwanzo.

Na Mwandishi Wetu.

Leave A Reply