Mbali na vyombo hivyo, jana asubuhi mwili huo ulifanyiwa uchunguzi ambao ulionyesha matundu manne ya risasi, moja kwenye mguu, mawili begani na jingine kwenye paji la uso ambako risasi iliingilia kichwani na haikuwa imetoka.
Chanzo cha habari katika Hospitali ya Mkoa wa Arusha, Mount Meru, ulikopelekwa mwili huo kilisema walipewa maagizo kuhakikisha hauondolewi hadi risasi iliyopo kichwani imeondolewa.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Profesa Jumanne Maghembe alisema Serikali inaendelea na uchunguzi ili kuwabaini majangili waliohusika.
Alivyouawa
Daily Mail lilisema jana kuwa inawezekana hata bunduki iliyomuua Gower ni ile waliyokuwa wanatumia majangili hao kuua tembo. Lilieleza kuwa wakati Gower akiwa katika doria, aliona mabaki ya tembo wawili chini.