NAHODHA wa Klabu ya Yanga, Nadir Haroub ‘Cannavaro’, leo Septemba 18, ameibuka katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar na kupata nafasi ya kuzungumza na aliyekuwa Mwenyekiti wa Klabu hiyo, Yusuf Manji.
Cannavaro Amfuata Manji Mahakama ya Kisutu
Baada ya kutinga mahakamani hapo, Cannavaro alimuwahi Manji na kusalimiana naye kisha kupiga kuzungumza mambo machache ambayo hata hivyo haijajulikana kama walikuwa wakijadili mambo ya soka kuhusu klabu hiyo au la!
Klabu ya Yanga imekuwa ikiongozwa na Manji kwa miaka mingi ambapo baada ya kushtakiwa na kuwekwa rumande kwa miezi kadhaa kabla ya wiki iliyopita kuachiwa huru kwenye kesi ya uhujumu uchumi.
Kesi ya Manji ya Matumizi ya Madawa ya Kulevya Yapigwa Kalenda
Baadhi ya mashabiki wa Yanga wamekuwa na shauku kubwa ya kuona Manji akiwa msitari wa mbele kuiongoza timu hiyo kama ilivyokuwa siku za nyuma.
Manji alikuwa mahakamani hapo kwa ajili ya kusikiliza kesi yake anayotuhumiwa kujihusisha na matumizi madawa ya kulevya ambayo hata hivyo imeshindwa kusikilizwa na kusogezwa mbele hadi Septemba 25 mwaka huu.