The House of Favourite Newspapers

Chadema watuma salamu za rambirambi kifo cha Leticia Nyerere

0

8-chademaCHAMA CHA DEMOKRASIA NA MAENDELEO (CHADEMA)

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI SALAAM ZA RAMBIRAMBI KIFO CHA LETICIA NYERERE

Tumepokea kwa masikitiko makubwa msiba wa Mhe. Leticia Nyerere uliotokea nchini Marekani.

Tunatoa pole kwa familia, ndugu, jamaa, marafiki katika wakati huu mgumu wa kuondokewa na mpendwa wao.

Mwenyezi Mungu awatie moyo wa ujasiri na subra katika wakati huu mgumu wa majonzi ya msiba huo.

Kama chama tutamkumbuka Marehemu Leticia kwa mchango wake na ushiriki wake wakati wote alipokuwa mwanachama wetu na akiwa miongoni mwa watu waliopata fursa za kuwa wabunge kupitia CHADEMA.

Bwana alitoa, bwana ametwaa, jina la Bwana lihimidiwe.

Imetolewa leo, Jumanne Januari 12, 2016 na;

Tumaini Makene

Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano
CHADEMA

Leave A Reply