The House of Favourite Newspapers

Chama Amaliza Mchezo Zambia

SIMBA tayari imefanikiwa kuwamaliza wapinzani wao Nkana FC nje ya uwanja na kilichobaki ni ndani ya uwanja, hiyo ni baada ya kufanikiwa kupangua fitna zao zote walizozipanga kabla ya mchezo wao wa Ligi ya Mabingwa Afrika, kesho Jumamosi.

 

Timu hizo zinatara­jiwa kuvaana kutafuta nafasi ya kucheza Hat­ua ya Makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, mchezo ukitarajiwa kupigwa mjini Kitwe, Lusaka nchini Zambia.

 

Simba ilifika hatua hiyo baada ya kuiondoa Mbabane Swallows ya Eswatini kwa jumla ya mabao 8-1, wakati Nkana ili­iondoa UD Songo ya Msumbiji kwa jumla ya mabao 3-1.

  Akizungumza na Cham­pioni Ijumaa, Mwenyekiti wa Bodi ya Simba, Swedy Mkwabi ambaye ameongo­zana na timu hiyo, alisema wanashukuru timu imefika salama Zambia na kupata mapokezi mazuri kutoka kwa wenyeji wao ambao ni Klabu ya Power Dynamos al­iyokuwa anaichezea kiungo wao, Clatous Chama.

 

Mkwabi alisema mapokezi hayo waliyapata tangu walipotua kwenye Uwanja wa Ndege wa Southdowns na kupokelewa na viongozi wa Power Dynamos kisha ku­wapeleka hotelini walipofikia.

Aliongeza kuwa, baada ya mapokezi hayo jioni walikwenda kufanya mazoezi kwenye Uwanja wa Dynamos ambao walipewa na wenyeji wao hao wa­naoutumia huku kukiwa na ulinzi mkali wa askari.

 

“Kilichobakia hivi sasa ni sisi wenyewe tushindwe kupata matokeo mazuri ugenini, lakini kuhusu fitna zilizokuwa zimepangwa tumejitahidi kuzikwepa kutokana na maandalizi tuli­yoyaweka ya kuwatanguliza baadhi ya viongozi wetu.

“Viongozi hao baada ya kufika huko waliandaa mapokezi mazuri kwa maana ya hoteli na kutu­andalia uwanja mzuri wa kufanyia mazoezi tuliyo­fanya jana (juzi Jumatano) na kesho (leo Ijumaa) huku tukipewa mlinzi mzuri na wenyeji wetu timu ya Power Dynamos.

 

“Pia, tunawashukuru Watanzania waishio hapa nchini Zambia ambao ni mashabiki wa Simba wame­kuwa wakitupa ushirikiano mzuri kiukweli, hivyo kili­chobaki hivi sasa ni kuwas­ubiri wapinzani wetu tutaka­pokutana uwanjani baada ya kufanikiwa kuzikwepa fitna,” alisema Mkwabi.

 

Katika msafara huo wa Simba uliongozwa na Mkurugenzi Mkuu wa Simba (C.E.O), Crescentius Magori pamoja na Mkuu wa Kitengo cha Habari na Mawasiliano wa Simba Haji Manara.

Stori: Ibrahim Mussa, Kitwe na Sweetbert Lukonge, Dar

MASHABIKI wa Simba Wacharuka Ndani ya Daladala Watu wapagawa

Comments are closed.