The House of Favourite Newspapers

Championi Latoa Misaada kwa Wagonjwa Hospitali ya Mwananyamala

Timu ya Championi ikiongozwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Global Group, Eric Shigongo,  wakiwasili katika Hospitali ya Mwanayamala jijini Dar es Salaam. Kulia ni Dr. Aileen Barongo ambaye ni Daktari Bingwa wa Watoto akiwapokea.

GAZETI namba moja la Michezo nchini Tanzania, la Championi kupitia kampeni yake ya Tuko Pamoja, leo Jumanne, Oktoba 1, 2019 limetembelea katika Hospitali ya Mwananyamala jijini Dar es Salaam na kutoa misaada kwa wagonjwa waliolazwa wodini.

 

Shigongo na Mhariri Mtendaji wa Global Publishers, Saleh Ally wakikabidhi msaada wa dawa kwa mmoja wa wazazi.

Wahariri na waandishi wa Championi walishiriki katika zoezi hilo wakiongozwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Global Group, Eric Shigongo pamoja na Mhariri Mtendaji wa Global Publishers, Saleh Ally.

…Akimjulia hali na kumbeba mmoja wa watoto wanaouguzwa hospitalini hapo.Timu ya Championi ilifika hospitalini hapo leo majira ya mchana na kutembelea wodi ya wazazi na watoto na kutoa misaada hiyo ikiwemo dawa, maji, juisi, pesa taslimu na vitu vingine vyenye uhitaji kwa wagonjwa hao.

…Akiwa na mmoja wa watoto waliokuwa wakipatiwa matibabu.

Akizungumza baada ya kukabidhi misaada hiyo, Saleh Ally, alisema:

Mwandishi wa Gazeti la Championi, Marco Mzumbe,  akimjulia hali mmoja wa watu wanaopata mataibabu na kumkabidhi biskuti kwa ajili ya mwanaye. 

“Hii ni kampeni ambayo imeanzishwa na Gazeti la Championi, tumeanzia Hospitali ya Mwananyamala, lakini pia tutaenda sehemu tofauti kwa watu wenye mahitaji maalum.

 

Mwandishi  Sharifa Mmasi (kulia),  akiwa na mmoja wa watoto waliolazwa hapo. 

“Haitakuwa kwenye hospitali pekee, bali hata kwenye vituo vya watoto yatima na wanamichezo, lengo ni kurudisha kwa jamii kile ambacho tunakipata.”

Awali wakati akikabidhi misaada hiyo na Timu ya Championi, Shigongo amewaasa akina mama hao waliokuwa wodini wakiuguza watoto wao na wengine wakijiuguza, kuwalea watoto wao katika misingi na maadili bora ili waje kuwa msaada kwao na taifa lao hapo baadaye.

Akizungumza ujio huo, mmoja wa akina mama hao, amelishukuru  Gazeti la Championi kwa misaada hiyo na kusema kuwa jambo hilo limekuwa ni faraja kubwa kwao, hivyo wanamuomba Mungu watumiapo dawa hizo ziwasaidie, wapone na warejee nyumbani kwa ajili ya kuendelea na shughuli zao za kila siku.

Mhariri wa Championi Jumatatu, Ezekiel Kitula (wa pili kulia), waandishi Wilbert Molandi na Ibrahim Mussa, wakimkabidhi maji na juisi mmoja wa wafanyakazi wa hospitali hiyo ikiwa ni sehemu ya kutambua ugumu na ubora wa kazi zao wanazozifanya kuokoa afya za Watanzania.

Mbali na kutoa misaada hiyo, Championi pia limefanya ukarabati wa jengo la Upasuaji Mkubwa (Main Theatre) katika hospitali hiyo kwa kulipaka rangi.

Mhariri wa Championi Ijumaa, John Joseph,  akimjulia hali na kumpa kinywaji mmoja wa watoto waliolazwa.

Championi Tuko Pamoja ni kampeni endelevu ya Championi ambayo itakuwa ikitoa misaada mbalimbali kulingana na uhitaji wa jamii.

Mmoja wa madaktari bingwa wa watoto katika Hospitali ya Mwananyamala, Aileen Barongo (kulia mbele) akiongozana na Mkurugenzi Mtendaji wa Global Group, Eric Shigongo (kushoto), Mhariri Mtendaji, Saleh Ally (katikati kwa nyuma), wakitembelea maeneo mbalimbali ya  hospitali hiyo zikiwemo wodi za watoto, wazazi na jengo la chumba cha upasuaji lililokuwa likikarabatiwa kwa udhamini wa programu maalum ya “Tuko Pamoja na Championi, leo.

 

Mmoja wa wagonjwa waliokuwa wakiuguzwa akitoa shukrani zake kwa uongozi wa Championi kwa msaada huo.

 

Baadhi ya waandishi na wahariri wa Gazeti namba moja la Michezo nchini la Championi wakiwa hospitalini hapo. 

 

Saleh Ally akimjulia hali na kumpa kinywaji mmoja wa watoto wanaopata matibabu.
Mhariri wa Gazeti la Championi Jumatano, Philip Nkini akimjulia hali na kumpa kinywaji mmoja wa watoto hospitalini hapo. 

 

Mwandishi wa Gazeti la Championi, Martha Mbona akimpa biskuti mtoto anayepata matibabu.

 

Mwandishi  Sharifa Mmasi akitoa juisi na misaada mingine kupitia kampeni ya “Championi Tuko Pamoja”  hospitalini hapo. 

 

Waandishi Ibrahim Mussa (kushoto) na Lunyamadizo wakishusha boksi lenye dawa ya kuchua (Salimia)  hospitalini hapo.

 

Shigongo akizungumza wakati wa kukabidhi misaada hiyo.

 

Timu ya Championi ikiwa na baadhi ya madaktari na wauguzi wa hospitali hiyo baada ya kukabidhi msaada huo kwa wagonjwa.

 

Saleh Ally akitoa msaada kwa mmoja wa watoto wanaotibiwa.

 

Mwandishi Wilbert Molandi (katikati) na Abraham Pacific wakijumuika na mmoja wa wazazi ambao watoto wao wamelazwa.

NA MUSA MATEJA

Comments are closed.