GAZETI la Championi limeanza kurejesha kidogo linachokipata kwa wasomaji wake, hivyo zawadi kemkemu zitamwagwa.
Msomaji atakayenunua gazeti hili na mengine ya Championi atakuwa na nafasi ya kujishindia fedha taslimu kuanzia shilingi 5,000, 10,000, 20,000, simu za mkononi na zawadi nyingine nyingi.
Unachotakiwa kufanya ni kununua gazeti, fungua ndani kwenye ukurasa mmoja utakuta stika ambayo imebandikwa, ifungue utakuta zawadi yako ndani, baada ya hapo piga simu kwenye namba iliyopo kwenye stika hiyo na ujitambulishe jina, umri, sehemu ulipo na zawadi uliyoshinda.
Baada ya hapo utapewa maelekezo ya jinsi ya kupata zawadi yako. Angalizo usipoteze gazeti wala kuponi uliyoshinda zawadi hiyo, kadiri unavyonunua magazeti mengi ndivyo unavyopata nafasi ya kushinda zawadi nyingi zaidi.
Hadi sasa washindi watatu wameshajinyakulia zawadi zao za fedha taslimu, ambao ni Nassor Gallu wa Dar aliyejishindia Sh 5,000, Moses Mwaige wa Mikocheni (Sh 10,000), Balari Likong’o wa Mbagala (Sh 5,000), John Bujiku wa Meatu (Sh 10,000) na Malumbano Peter wa Arusha (Sh 10,000).
MWANDISHI WETU, Dar es Salaam
Comments are closed.