MAGAZETI ya Championi na Uwazi yanayochapishwa na Kampuni kongwe na bora ya Magazeti Afrika Mashariki, Global Publishers jana Jumanne, Januari 29, 2019, yamegawa zawadi za tisheti kwa wauzaji wake na wasomaji wa magazeti hayo katika maeneo mbalimbali ya jiji la Dar es Salaam.
Zawadi hizo ni mwendelezo wa promosheni zakeĀ kabambe ambazo wateja wa magazeti hayo wanajishindia pesa taslim kuanzia Tsh. 10,000 hadi Tsh. 100,000 na wengine wakiibuka washindi wa simu za kisasa kila wiki kwa kununua magazeti hayo, jana yalikuwa kwenye mitaa ya Bunju B, Kigamboni, Mbagala, Gongo la Mboto na Mabibo jijini Dar es salaam ambapo wauzaji wake walipata fursa ya kuzawadiwa tisheti za Championi na za Uwazi.
Mbali na tisheti hizo, timu ya masoko ya Global Publishers iliwahamaisha wasomaji wake kununua Championi na Uwazi ambayo ndani yake yanatoa fursa ya msomaji kushinda zawadi hizo.
Kwa Championi kuna stika maalum yenye zawadi ambazo ni simu na pesa taslim, hivyo msomaji akinunua gazeti hilo anapaswa kuangalia ndani iwapo atakuta stika ya zawadi ailete ofisini kwetu Sinza Mori akiwa na gazeti lake, ataopewa zawadi ya mkwanja au simu jannja (smartphone) mpya papo hapo.
Kwa upande wa Uwazi, unaponunua gazeti hili kuna kuponi na maelezo ya namna ya kushiriki katika ukurasa wa pili wa gazeti hilo, hivyo unahimizwa kununua Uwazi na kushiriki promosheni hiyo ambayo itakufanya uibuke na mkwanja mrefu hasa katika kipindi hiki kigumu cha mwanzo wa mwaka ambapo hali ya uchumi ni ngumu ama simu janja mpya kwa ajili ya mawasiliano.
Hata wewe unaweza kuwa mshindi, wengi wamekuwa washindi kwa kuchukua uamuzi wa kusoma magazeti yanayochapishwa na Global Publishers.
Wewe unaweza kujishindia zawadi kemukemu kwa kununua gazeti la Championi na Uwazi, lakini magazeti mengine ya Global Publishers ambayo ni Risasi, Amani, Ijumaa na Ijumaa Wikienda yanakupa nafasi ya kujishindia zawadi za T-shirt, fedha taslimu na zawadi nyingine nyingi ambazo zinapatikana kwa kununua magazeti hayo kwa shilingi mia nane (800) tu, ukajinyakulia zawadi zawadi mbalimbali.
Na Musa Mgema, Dar es Salaam
Comments are closed.