Chelsea Yaitungua Watford
Chelsea wameendelea kusalia kileleni mwa msimamo wa EPL baada ya kufanikiwa kuibuka na ushindi wa 2-1 ugenini dhidi ya Watford katika muendelezo wa ligi kuu soka nchini England.
Mabao ya Mason Mount na kiungo Hakim Ziyech yalitosha kuipa alama zote tatu Chelsea katika mchezo huo uliokuwa na ushindani wa kipekee.