WAKONGWE kwenye game ya Bongo Fleva, Chid Benz na Q Chilla wamefanya makamuzi ya aina yake wakati wa Tamasha la Wiki ya Usalama Barabarani linalofanyika leo Jumamosi katika Uwanja wa Taifa, jijini Dar es Salaam.
Katika tamasha hilo lililoandaliwa na Wizara ya Mambo ya Ndani ya nchi kitengo cha Usalama Barabarani likiwashirikisha wasanii mbalimbali wa muziki na filamu hapa nchini, lengo kubwa ni kutoa elimu juu ya usalama barabarani ili kupunguza ajali.
Chila na Chid wamekiwasha huku wakishangiliwa maelfu ya mashabiki waliofurika kwenye Tamasha hilo.
Wakali hao wa tangu kitambo hicho, waliamsha hisia zaidi za mashabiki wao baada ya kugonga ngoma yao mpya ya Muda ambayo wameiachia hivi karibuni na kupokelewa vizuri sokoni.
NA DENIS MTIMA | GPL