The House of Favourite Newspapers

Choki: Napumzika na Familia Yangu Kwanza

Ally Choki.

 

BAADA ya kumaliza mkataba na Bendi ya The African ‘Twanga Pepeta’, mwanamuziki Ally Choki amefunguka kuwa, hana mpango wa kuanzisha bendi kama alivyosema mwanzoni, bali anapumzika na kuangalia familia yake huku akiwa anafanya kazi na bendi nyingine.

 

Akibonga na Risasi Vibes, Choki alisema kuwa, anafanya kazi na Bendi ya The Mafiki huku muda mwingi akiutumia kwa ajili ya kuangalia familia zaidi na kuhofia kuanzisha bendi yake kutokana na hali halisi ya sasa, kwamba, muziki huo haulipi na bendi alishakuwa nayo, ikafa.

 

“Mwanzoni nilitamani kuirudisha bendi yangu ya Extra Bongo, lakini nimekuja kutafakari nikaamua niachane nayo tu maana nitaumia zaidi kwani kuwa na bendi kuna changamoto kubwa sana hivyo nitaendelea kufanya kazi na bendi za watu na kutulia na familia zaidi,” alisema.

Risasi Vibes

Comments are closed.