The House of Favourite Newspapers

Chris Brown Kumrudia Rihanna

0
Mkali wa Muziki wa Pop, Christopher Maurice ‘Chris Brown’ akiwa na Rihanna.

TAARIFA kutoka chini ya kapeti zinaeleza kuwa, miezi michache baada ya kutengeneza filamu fupi ya maisha yake, mkali wa Muziki wa Pop, Christopher Maurice ‘Chris Brown’ huenda akarudiana na aliyewahi kuwa mpenzi wake, Rihanna.

Kwa mujibu wa chanzo cha karibu na Chris, baada ya filamu hiyo kutoka inayoitwa Welcome To My Life, Chris anaamini kwa asilimia kubwa Rihanna ameiona yote na atakuwa tayari kurudiana naye. “Chris anaamini Rihanna ameshamsamehe baada ya kuangalia filamu.

 

Chris alishawahi kumwambia rafiki yake anataka kuwa anamchukua Rihanna na kwenda naye kwenye filamu,” kilisema chanzo.

H Baba, Flora Mvungi Utajiri Nje Nje!! Mtoto Wao Alamba Dili Nono


Leave A Reply