The House of Favourite Newspapers

Chuchu: Kubadilisha Jina Sio Kumuacha Ray

MSANII wa filamu za Kibongo, Chuchu Hans ameibuka na kusema kuwa tetesi zilizozagaa akidaiwa kuachana na mzazi mwenziye Vincent Kigosi ‘Ray’ na kwamba ndiyo sababu ya kubadili jina lake kwenye ukurasa wake wa Instagram siyo za kweli.

Awali kwenye ukurasa wa Insta Chuchu alikuwa akijiita Chuchu Hans the Great na sasa anajiita Chuhans Kichuna, jambo lililowafanya wengi waamini safari ya mapenzi yao imefika mwisho.

Akizungumza na Risasi Jumamosi, Chuchu alisema kuwa yeye ameamua tu kubadili jina na wala hajaachana na Ray na kama wapo wanaosubiri penzi livunjike, watasubiri sana.

“Waniache jamani kila siku nimeachana na Ray… nimeachana na Ray…, nina sababu zangu za kubadilisha jina, haina maana kwamba tumeachana, hata hivyo sitaki kuongelea sana suala hilo kama tumeachana au la, majibu mtayapata subirini tu,”alisema Chuchu.

 

STORI: MAYASA MARIWATA

Comments are closed.