The House of Favourite Newspapers
gunners X

Chuchu: Mtoto Ameongeza Mahaba kwa ‘Baby’

ray-4STORI: IMELDA MTEMA | RISASI

MUIGIZAJI wa sinema za Kibongo, Chuchu Hans ambaye hivi karibuni alijifungua mtoto wa kiume (Jayden), amesema mtoto huyo ameboresha mahaba niue kwa mpenzi wake, Vincent Kigosi ‘Ray’.

Akizungumza na Mikito Nusunusu, Chuchu alisema mtoto huyo amekuwa ni faraja kwao wote na mapenzi yameongezeka baina yake na mpenzi wake huyo kitu ambacho anamshukuru Mungu.

“Jamani mwacheni Mungu aitwe Mungu, mahaba yamezidi asilimia ni jambo la kumshukuru sana aliye juu maana bila yeye kusingekuwa na kitu kabisa na ninamuomba atimize mambo mengine makubwa zaidi,” alisema Chuchu.

Shinda Nyumba Awamu ya Pili Yatikisa Jiji la Dar es Salaam

Comments are closed.