Kampuni ya Coca Cola Tanzania, imezindua kampeni ya Sisimua Maisha na Fanta katika hafla iliyopambwa na burudani mbalimbali jijini Dar es Salaam.
Katika uzinduzi huo, wapenzi wa kinywaji hicho, walipata fursa ya kushiriki burudani na michezo mbalimbali kabla ya kuingia kwenye treni linalofanya safari kati ya Ubungo na Stesheni ambalo lilikua na chapa na rangi mbalimbali za Fanta.
Kabula Nshimo ambaye ni Meneja Masoko wa Cocacola Tanzania, amesema lengo la kuzindua kampeni ya Sisimua Maisha na Fanta ni kuwaleta pamoja wapenzi wa kinywaji hicho na kuwahamasisha watu wengine kuendelea kunywa soda hiyo maarufu lakini pia kuwahamasisha kushiriki kwenye michezo na burudani mbalimbali kila wanapopata nafasi.
Na Mwandishi Wetu