IKIWA ni saa chache baada ya video kusambaa katika Mitandao ya Kijamii ikionyesha askari mgambo wakimpiga kijana Robson Orotho anayedaiwa kutolipa faini ya usafi, watuhumiwa wa kosa hilo wamematwa jijini Dar es Salaam.
Kwa mujibu wa taarifa ya Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es salaam, waliokamatwa ni Kelvin Edson, Gudluck Festo, Rehema Nyange. Watafikishwa Mahakamani haraka iwezekanavyo.
Comments are closed.