Sharif Ramadhani ‘Darasa’
BONIPHACE NGUMIJE
MWANAMUZIKI wa Hip Hop Bongo anayetamba na Ngoma ya Too Much, Sharif Ramadhani ‘Darasa’ amefunguka kuwa bila yeye kumshirikisha msanii wa Bongo Fleva, Rich Mavoko kwenye ngoma yake ya Kama Utanipenda angepotea kimuziki.
Rich Mavoko
Akich-onga na Showbiz Xtra, Darasa alisema kuwa Mavoko ni mkali lakini kuna wakati ulifika akaanza kama kupoteza nguvu aliyokuwa nayo kwenye gemu hivyo baada ya kumshir-ikisha kwenye wimbo wake huo amerudi kwenye reli
jambo ambalo anajivunia.
“Sikatai kuwa Mavoko ni mkali, lakini hakuna asiyefahamu kuwa kuna wakati alianza kama kupotea hivi kwenye gemu na mimi ndiye niliyemrudisha tena baada ya kumshirikisha kwenye wimbo wangu, Kama Utanipenda!” alisema Darasa.