The House of Favourite Newspapers

Darleen: Nilikuwa Chauroho Ile Mbaya

IMEFUNUKA! Ndivyo ambavyo un­aweza kusema baada ya mwanamuziki kuto­ka Lebo ya Wasafi Classic Baby (WCB) Mwanahawa Abdul ‘Queen Darleen’ ku­funguka kuwa, alipokuwa mdogo alikuwa chau­roho kwani alipenda sana kukomba chakula akiwa anakula na watu wengi.

 

Akizungumza na Ijumaa Wikienda, Dar­leen alisema alifikia hatua ya kuonekana na tabia hiyo kwani kila al­ipokuwa anakula kwenye sahani au sinia na wen­zake, alikuwa akikomba chakula na kujikusanyia upande wake.

 

“Nilikuwa na tabia mbaya sana, yaani tukiwa tunakula wengi kwenye sinia halafu nione kama wananizidi spidi, naanza kukomba chakula, najiku­sanyia upande wangu yaani nilikuwa mroho kupitiliza, ila mama yangu aliikome­sha hiyo tabia kwa sababu ilikuwa ikitia aibu mbele za watu,” alifichua Darleen huku akicheka.

Stori: Shamuma Awadhi

Comments are closed.