The House of Favourite Newspapers

Davido: Spimi Tena DNA


STORI: LAGOS, NIGERIA | SHOWBIZ | UWAZI

MKALI wa Miondoko ya Afro Pop, kutoka Nigeria, David Adeleke ‘Davido’ hivi karibuni ameweka wazi kuwa hawezi kufanya tena vipimo vya DNA ili kuthibitisha kuwa mtoto wa kike Veronica ni wake baada ya vipimo alivyofanya awali kuonyesha kuwa si damu yake.

 

Akizungumza na vyombo vya habari Nigeria hivi karibuni, Davido aliongeza kuwa mama wa mtoto huyo, anayefahamika kwa jina la Abadan alimpakazia juu ya ujauzito huo na kwamba haukuwa wake jambo alilolielewa tangu awali lakini alitaka tu kuwaridhisha watu ambao hawakuwa wanaamini juu ya hilo kwa kupima DNA.

“Vipimo vya DNA haviwezi kudanganya, huyo mwanaume ni mpigaji tu, anataka pesa za haraka na umaarufu, siwezi kurudia kufanya vipimo hivyo, kwa sasa nipo bize na mambo yangu binafsi,” alimaliza Davido.

Comments are closed.