STAA wa filamu Bongo Halima Yahya ‘Davina’ amemlipua mwanamitindo maarufu, Hamisa Mobetto kutokana na ishu ya kuzaa na Mbongo Fleva ambaye ni mwandani wa Zarina Hassan ‘Zari Boss Lady’.
Akizungumza na Star Mix kutokana na sekeseke hilo baada ya mwanamuziki huyo kuweka wazi kwamba ni kweli mtoto huyo ni wake alisema, kitu ambacho anakiona wote wawili wana makosa, iweje Mbongo Fleva huyo alale na mtu mwingine kitanda anacholala na mwanamke wake, pia kwa nini Mobetto alikubali kulalia kitanda hicho bila huruma kwa mwanamke mwenziye.
“Hili swala kilichonifurahisha ni baada ya huyo mwanaume kukiri kumzalisha Hamisa, lakini nikiongea kwa kumshauri kama mwanamke mwenzangu, hata kama alikuwa naye hakupaswa kukubali kulalia kitanda kimoja,” alisema.