MKUU wa Wilaya ya Ilala, Sophia Mjema, leo amezindua utaratibu maalumu wa kuwatambua wafanyabiashara wadogowadogo maarufu kama Wamachinga kwa kuwapatia vitambulisho vya taifa ili watambulike katika mabenki wakati wa kuomba mikopo kwa ajili ya kupanua wigo wa biashara zao.
Akizungumza katika uzinduzi huo katika soko la Kariakoo, Dar es Salaam, Mjema amesema serikali ya awamu ya tano inataka kuona wafanyabiashara hao wanakua kiuchumi na hivyo na hivyo kuwapa uwezo wa kukopa katika mabenki kutokana na vitambulisho hivyo.
Naye mfanyabiashara katika soko la Kariakoo, John Mushi, ameipongeza hatua hiyo ya serikali kwani itasaidia kupunguza migogoro kati yao na mgambo wa jiji.
Comments are closed.