Mhariri Mtendaji wa Global Publishers, Richard Manyota (kulia) akimfariji Edwin Isaac aliyefiwa na shangazi yake.
Waombolezaji akiwa katika foleni kusubiri mwili wa marehemu kushushwa kwenye gari.
Mmoja wa wanandugu akiwa na shada la maua baada ya mwili wa marehemu kushushwa kwenye gari.
Ndugu wa marehemu (mwenye msalaba) akiwaongoza waombolezaji waliokuwa wamebeba jeneza lenye mwili wa marehemu kwenda ndani.
Waombolezaji wakitoa sadaka wakati wa kuuaga mwili wa marehemu.
Dereva wa Kampuni ya Global Publishers, Edwin Isaac amepata pigo baada ya kufiwa na shangazi yake Bi Agnes Lwidiko Msemwa (84) aliyefariki jana katika Hospitali ya Amana jijini Dar es Salaam.
Mwili wa marehemu umeagwa leo Tabata Chang’ombe wilayani Ilala, Dar na kusafirishwa kwenda Njombe kwa mazishi. Mhariri Mtendaji, Richard Manyota alihudhuria kumwakilisha Mkurugenzi Mtendaji wa Global Publishers, Eric Shigongo.
(PICHA NA MAKONGORO OGING)