The House of Favourite Newspapers

Diamond Yamkuta ya Wema… Atimuliwa Kwenye Nyumba ya Studio

0

DIAMOND-1.jpgStaa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond.

Musa Mateja

SIKU chache baada ya muigizaji kiwango Bongo, Wema Sepetu ‘Madam’ kutimuliwa katika nyumba aliyokuwa amepanga maeneo ya Kijitonyama jijini Dar es Salaam kwa kosa la kutolipa bili ya umeme na maji, Jumatano hii, zilipendwa wake, Nasibu Abdul ‘Diamond’ naye alikutana na kimbembe kama hicho kutoka kwa mmiliki wa nyumba aliyokuwa akiitumia kama studio, iliyopo Sinza Mori, Risasi Jumamosi linakuhabarisha.

Diamond Studio (1)-001Jengo la studio hiyo

Kwa nyakati tofauti, chanzo kinasema majirani waliwahi kupanda juu ya uzio wa nyumba hiyo na kutaka kupunguzwa kwa sauti ya muziki, lakini Diamond na madansa wake wamekuwa wakikaidi kwa madai kuwa hiyo ni sehemu ya kazi yao, jambo lililosababisha kuwasiliana na mmiliki wa nyumba hiyo ili amtoe msanii huyo, vinginevyo watamshtaki.

Diamond Studio (3)-001“Jamaa baada ya kuitwa na mwenye nyumba na kuambiwa kuhusu jambo hilo na kutakiwa kuhama, aliongea naye kutaka amuuzie kabisa nyumba hiyo lakini akakataa na hata alipong’ang’ania, Diamond alitajiwa bei isiyofanana hata kidogo na nyumba hiyo, akaondoka usiku-usiku kama ilivyokuwa kwa Wema kukwepa aibu,” kilisema chanzo chetu.

Diamond Studio (2)-001Gazeti hili liliwasiliana na msanii huyo ili kupata ukweli wa tukio hilo lakini alikataa kuzungumzia lolote juu ya ishu hiyo. Uchunguzi wa gazeti hili umebaini kuwa staa huyo amehamishia ofisi zake eneo la Sinza Mapambano, hatua chache tu kutoka alipotimuliwa.

Leave A Reply