Diamond Akutana Na Busta Rhymes, Swizz Beats Studio -Video
Rapa Legendary kutokea nchini Marekani Busta Rhymes ameshare video akiwa na Mwanamuziki wa Tanzania, Nassib Abdul maarufu Diamond Platnumz wakiwa Studio na kumwagia sifa kibao ikiwemo kumuita ‘Michael Jackson of Africa’, yaani Michael Jackson wa Afrika.
Katika video hiyo ambayo wanaonekana kama wanasuka mdundo wa pamoja, wameonekana mastaa wengine akiwemo Swizzle.
Diamond amedai kuwa atakua nchini Marekani kwa muda ili kuandaa Album yake, ambayo Producer wake Mkuu anatokea nchini humo (hakutaja jina lake).