The House of Favourite Newspapers

DIAMOND ATUA SUMBAWANGA KWA NDEGE, MAPOKEZI YAKE BALAA! (VIDEO & PICHA)

Ndege iliyowabeba Wasafi ikitua Uwanja wa Sumbawanga.

STAA wa Bongo Fleva, Diamond Platniumz na crew yake ya kutoka Lebo ya Wasafi leo wamewasili mjini Sumbawanga kwa ajili ya Tamasha la Wasafi Festival linalotarajiwa kufanyika kesho Jumamosi katika Uwanja wa Mandela mkoani humo.

Meneja wa Wasafi, Bab Tale akiwa katika pozi la kuweka mambo sawa kabla ya wasanii wake kushuka.

Msanii huyo na kundi lake wametua Sumbawanga kwa ndege na kupata mapokezi ya aina yake ambapo barabara zote alizopita msanii huyo ilibidi zifungwe kwa muda mpaka alivyopita huku msafara huo ukisindikizwa na mashabiki hadi kwenye hoteli aliyofikia.

Lavalava akishuka.
Mboso.

 

Rayvany akiwapa hai mashabiki wakati akishuka.
Hivi ndivyo Queen Darlin alivyoshuka.
Hivi ndivyo Diamond alivyojitokeza mbele ya umati uliofika uwanja wa ndege kumpokea.

 

Hivi ndivyo mabaunsa walivyopata tabu kumpeleka kwenye gari kila shabiki akitaka kumuona kiukaribu na wengine kumgusa Diamond.
Mashabiki wengine wakiunga msafara kwa miguu wengine bodaboda.

 

Diamond na wasanii wake wakiwa kwenye gari la matangazo wakizunguuka mitaa ya Sumbawanga.
Umati ukiwa umezingira msafara katika moja ya mitaa ya Sumbawanga.

PICHA: RICHARD BUKOS / GPL

ITAZAME VIDEO YA MAPOKEZI YAKE

                  PART 1

 

 

                 PART 2

 

Comments are closed.