The House of Favourite Newspapers

Diamond, Kajala mahaba niue!

0

Diamondss-2.jpgStaa nambari moja Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’.

Musa Mateja

NI gumzo! Ubuyu motomoto ambao unasambaa kwa kasi ya ajabu kama moto wa kifuu mjini unadai kuwa,  staa nambari moja Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ na mwigizaji Kajala Masanja wamedaiwa kuwa ni wapenzi na sasa ni mahaba niue, Risasi Jumamosi limesheheni full stori.

TUJIUNGE NA CHANZO

Kwa mujibu wa chanzo makini, uhusiano wa Diamond na Kajala  unadaiwa kuibuka ghafla miezi kadhaa iliyopita lakini wamekuwa wakifanya siri nzito kabla ya hivi karibuni kukolea zaidi baada ya mpenzi wa Diamond, Zarina Hassan ‘Zari The Boss Lady’ kurudi nchini mwake, Afrika Kusini ‘Sauz’.

“Walianza zile za kimjinimjini, wakawa wanafanya yao kimyakimya tangu Zari akiwepo lakini mahaba niue yamekuja kushamiri zaidi baada ya Zari kutimkia zake Sauz,” kilisema chanzo chetu.

kajala.jpgMwigizaji Kajala Masanja.

MASTAA WAZUNGUMZIA

Mara baada ya chanzo hicho kumwaga ubuyu huo, Risasi Jumamosi lilipenyezewa data kutoka kwa mastaa tofauti ambao wanafahamu uhusiano huo mpya ambao pia ulianza kusambaa taratibu katika mitandao ya kijamii.

“Hivi kwani nyinyi hamjaipata habari hii? Diamond amemnasa Kajala na mambo yao ni bambam. Sema kiukweli Diamond ni msiri maana unajua ana mambo mengi hivyo hapendi kabisa hii ishu ijulikane,” alisema staa mmoja mkubwa Bongo huku akiomba hifadhi ya jina.

zari3.jpgMpenzi wa Diamond, Zarina Hassan ‘Zari The Boss Lady’.

Kama hiyo haitoshi, staa mwingine aliliambia Risasi Jumamosi kuwa, dada wa Diamond, Esma anaujua mchezo mzima na anatajwa kuusambaza ubuyu huo kama malipo kwa Wema (Sepetu) anayemtuhumu kumuibia bwana wake, Petit Man.

“Esma ameamua kumwaga ugali maana Wema na timu yake wamekuwa wakijitapa sana mjini kwamba wamemnyakua mume wa Esma, Petit Man. Na yeye anawaonesha kwamba kama ni kuchukuliwa mbona hata Kajala amechukuliwa na Diamond ambaye alikuwa mtu wa Wema lakini wamekaa kimya,” alisema msanii huyo.

Jitihada za kumpata Esma ili aweze kuzungumzia suala hilo ziligonga mwamba baada ya simu yake ya mkononi kuita muda mrefu bila kupokelewa.

MITANDAO YAZIDI KUKUZA JAMBO

Mpaka tunakwenda mitamboni, juzi, mitandao mbalimbali hususan Instagram, wadau walisambaza habari ya Kajala na Diamond huku wakijaribu kumwambia Zari amtambue Kajala kama mke mwenzie kwani ameshalala Madale, nyumbani kwa Diamond.

“Zari mke mwenzio ni huyu hapa, anakusaidia. Juzi amelala Madale na Diamond,” iliandikwa na mdau mmoja wa Instangram.

ZARI ACHANGANYIKIWA

Chanzo kilichomwaga ubuyu huo kimeeleza kuwa, taarifa za Kajala na Diamond zilipomfikia Zari, alichanganyikiwa na kuanza kumcharukia Diamond au baba Tiffah ambaye ilibidi atumie nguvu ya ziada kumtuliza kwani bado wawili hao wanaendeleza uhusiano wao huku wakijua Zari hayupo Bongo.

“Zari alicharuka kwelikweli. Ilibidi Diamond atumie nguvu ya ziada kumtuliza na bahati nzuri mtoto wa kike ameelewa,” kilisema chanzo chetu.

DIAMOND SASA

Alipotafutwa Diamond na kusomewa mashitaka yake, mambo yalikuwa hivi:

Risasi Jumamosi: Kuna taarifa kwamba unatembea na Kajala na sasa mahaba ni motomoto, vipi kuna ukweli? Tena vyanzo vingine vinadai kuna hadi picha za wewe na Kajala mkiwa nyumbani kwako, unazungumziaje hilo?

Diamond: Aaah! Siyo kweli mwanangu…picha kweli mnazo? Picha gani…yaani kiaje?

Risasi Jumamosi: Inasemekana zipo ambazo mpo nyumbani kwako, Madale.

Diamond: Aahaha! Aaah uongo mtupu siyo kweli. Kama kuna picha kweli nitumieni basi.

KAJALA SASA

Alipopigiwa simu zaidi ya mara tano, Kajala hakupokea. Risasi Jumamosi lilimtumia ujumbe mfupi wa maneno (SMS) uliosomeka hivi:

“Habari, kuna ishu yako hapa Global Publishers, inahusu madai ya wewe kutoka kimapenzi na Diamond jambo ambalo linadaiwa kuleta mtafaruku mkubwa kati yako na Zari. Pia hata kwenye mitandao ya kijamii bila shaka umesikia, naomba ufafanuzi wako tafadhari.”

Licha ya ujumbe huo kuonesha kumfikia, hadi tunakwenda mitamboni, Kajala hakujibu chochote.

KAMA NI HIVYO

Madai ya kuwepo kwa uhusiano huo yanaweza kumweka Kajala katika mtazamo mwingine kijamii, kwani miaka miwili nyuma alidaiwa kutoka kimapenzi na mwanaume anayeitwa CK ambaye hakuna shaka alikuwa mpenzi wa Wema kabla ya kumwagana.

Hali hiyo ilizua mjadala, Kajala alibebeshwa madai mazito kwamba alikuwa na uhusiano na CK hata akiwa na Wema, ikitafsiriwa kwamba alikuwa akimlia vyake mwenzake hali iliyozua mgogoro wa wawili hao.

Diamond naye, amewahi kuwa na uhusiano wa kimapenzi na Wema, wakamwagana. Kitendo cha kudaiwa kutoka na Kajala, kinazidi kumweka mdada huyo katika mlolongo wa kudhaniwa anamwandama Wema kwa vile kila alikopita, yeye naye anapita!

Leave A Reply