Diamond Uso kwa uso na Young Thug
Staa wa Ngoma ya Nana, Nasibu Abdul ‘Diamond’.
Rapa kutoka Marekani, Jeffrey Lamar Williams ‘Young Thug’.
STAA wa Ngoma ya Nana, Nasibu Abdul ‘Diamond’ amekuwa msanii wa kwanza kutoka Afrika Mashariki aliyetajwa kutumbuiza kwenye Tamasha la BET Experience Africa ambapo atajumuishwa na rapa kutoka Marekani, Jeffrey Lamar Williams ‘Young Thug’.
Tamasha hilo litakalofanyika Desemba 12, mwaka huu katika Jiji la Johannesburg, litakuwa la kwanza kufanyika katika ardhi ya Afrika.
Hadi sasa ‘watakaopafomu’ kwenye tamasha hilo ni Flavour, AKA, Tamar Braxton na Maxwell ambapo orodha bado itaendelea kutangazwa.