The House of Favourite Newspapers

Diamond: Wema, Mobeto na Tunda ni Familia Yangu

Wema Sepetu.

MKURUGENZI wa lebo ya Wasafi Classic Baby ‘WCB’, Diamond, amefungukia ishu yake na mastaa watatu, Wema Sepetu, Hamisa Mobeto na Tunda Sabasita.

 

Amesisitiza kuwa urafiki wao umepitiliza kiasi cha kuwa sehemu ya familia yake. Akizungumza na Spoti Xtra, Diamond alisema kwamba wasanii hao hayuko nao kimapenzi tena.

Mkurugenzi wa lebo ya Wasafi Classic Baby ‘WCB’, Diamond.

“Kikubwa watu wanatakiwa watambue kwamba Wema alikuwa mpenzi wangu enzi hizo lakini kwa sasa hatuna mapenzi zaidi ya kuwa marafiki waliyopitiliza, kwani tuko kama ndugu.

                                               Hamisa Mobeto.

“Kwa maana hiyo utagundua wazi kuwa hata huko nyuma tulikuwa tukigombanishwa zaidi na mashabiki zetu jambo ambalo sasa haliwezi kujirudia kwa sababu tumeshakua watu wazima.

Tunda Sabasita

“Suala la Tunda linasemwa sana ila ukweli ni kwamba hata yeye ni rafiki yangu mkubwa na ndiyo maana anaonekana sana katika familia yangu, suala la Mobeto lipo wazi kabisa kuwa ni mzazi mwenzangu hivyo naye atabaki kama rafiki wa karibu tu kwa kila jambo letu linapotokea.

 

“Pamoja na kwamba juzi hakutokea katika utambulisho wa Maromboso kwani kadi ya mwaliko tulimpa sema hakuja kutokana na kupata dharura,” alisema Diam-ond.

Comments are closed.