Dida afungua tawi Bongo
Mmiliki wa studio hiyo Dida akiwa na baadhi wa wasanii wake
Waongozaji wa studio hiyo wakiwa na vitu mbalimbali.
Baadhi ya wasanii ambao wapo ndani ya Dida Entertainment.
Mwanaharakati na mdau mkubwa wa filamu ambaye pia ni mmiliki wa Dida Entertainment, Hadija Seif ‘Dida’ ambaye hapo hawali alikuwa akifanya shughuli zake za burudani nchini Uingereza, hivi karibuni amefungua studio yake hapa nchini ambapo amewakusanya wasanii mbalimbali wa Bongo.
Akizungumza na mtandao huu kwenye ofisi yake hiyo iliyopo Magomeni Dar, Dida alisema kuwa studio aliyofungua itakuwa ikifanya vitu vingi kama kurekodi na pia kutakuwa na Dida’s Online Tv na vitu vingine vingi.