The House of Favourite Newspapers

DK TULIA AICHAMBUA SERIKALI YA JPM, UNUNUZI WA NDEGE

Dk Tulia Ackson akizungumza na baadhi ya wafanyakazi wa Global Group katika ofisi za makampuni hayo zilizopo Sinza-Mori jijini Dar es Salaam, leo.

NAIBU Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk Tulia Ackson Mwansasu, amesema Serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Rais Dk John Pombe Magufuli (JPM), inalenga zaidi kwenye matokeo ya utekelezaji wa miradi mikubwa, ikiwemo ununuzi wa ndege.

 

Dk Tulia akiwasili katika ofisi za Global Group.

 

Dk Tulia amesema Rais Magufuli ni mtu anayependa kuona mambo mliyokubaliana yakitendeka badala ya maneno tupu na ndiyo maana katika utawala wake, mambo makubwa ambayo awali yalikuwa hayawezekani, sasa yanatekelezwa na Serikali yake.

Dk Tulia akisalimiana na Mkurugenzi wa Global, Lydia Bukumbi.

 

Dk Tulia akisalimiana na Meneja Mkuu wa Global, Abdallah Mrisho.

Dk Tulia ameyasema hayo mapema leo asubuhi alipotembelea ofisi za Global Group zilizopo Sinza-Mori jijini Dar, kampuni inayohusika na uendeshaji wa mtandao huu, Chaneli ya Global TV Online na wachapishaji wa Magazeti ya Championi, Ijumaa, Ijumaa Wikienda, Amani, Risasi, Uwazi, Spoti Xtra na Betika na kuongeza kwamba watu wanaopinga hatua zinazochukuliwa na Rais Magufuli, wanatakiwa kuelimishwa.

Mhariri wa Gazeti la Uwazi, Amrani Kaima akimwonesha Dk Tulia gazeti hilo.

“Tukizungumzia ununuzi wa ndege kwa mfano, baadhi ya watu wanaweza kuhoji kwamba tutanufaika nini na ndege bila kujua kwamba zitatumika kuwaleta watalii ambao wataleta fedha nchini kwetu ambazo zitasambaa kwenye mzunguko na kumfikia kila mmoja.

Mhariri Mtendaji wa Global Publishers, Saleh Ally (kulia) akimwonesha Dk Tulia, magazeti ya Championi.

Mfanyabiashara anataka wateja, wafanyakazi wanataka mishahara, hizo fedha zote lazima ziwepo kwenye mzunguko na watalii watakaoletwa na ndege zetu ndiyo watakaoingiza fedha hizo, kwa hiyo ni suala la kuelimishana tu, lakini ninampongeza sana mheshimiwa Rais kwa hatua anazozichukua.

Mhariri wa Gazeti la Ijumaa, Sifael Paul akimuuliza swali Dk Tulia.

“Mtu mwingine anaweza asione umuhimu wa ujenzi wa mradi wa Stiegler’s Gorge wakati anatumia umeme, hata yule ambaye anatumia mafuta ya taa ili apate mafuta ni lazima yasafirishwe, lazima yapite kwenye barabara, kwa hiyo utagundua kwamba juhudi za mheshimiwa Rais zinagusa maisha ya watu wengi zaidi,” alisema Dk Tulia.

Dk Tulia akizungumza na wafanyakazi wa Global, hawapo pichani.

 

Dk Tulia ndani ya studio za +255 Global Radio.

 

Dk Tulia ndani ya studio za +255 Global Radio.

 

Dk Tulia ndani ya studio za +255 Global Radio.

 

Mrisho akimwonesha Dk Tulia, tuzo ya Silver Play Button ambayo YouTube iliitunuku Channel ya Global TV Online baada ya kufikisha subscribers laki moja (100,000).

 

Mrisho akimwonesha Dk Tulia, tuzo ya Gold Play Button ambayo YouTube iliitunuku Channel ya Global TV Online baada ya kufikisha subscribers milioni moja (1,000,000).

 

 

Dk Tulia na timu ya +255 Global Radio.

 

Dk Tulia ndani ya Studio za Global TV Online.

 

Dk Tulia katika picha ya pamoja na baadhi ya wafanyakazi wa Global Group.

 

PICHA: MUSA MATEJA na SWEETBERT LUKONGE | GLOBAL PUBLISHERS

Comments are closed.