The House of Favourite Newspapers

Donald Trump Sasa Rasmi Kugombea Urais Marekani

0

mary-pat-christie-donald-trump

Donald Trump ateuliwa kuwa mgombea urais kwa tiketi ya chama cha Republican, uchaguzi unaotarajiwa kufanyika mwezi Novembea mwaka huu. Trump amepata uungwaji mkono na wajumbe kutoka majimbo na wilaya za Marekani katika kura mchujo wa kumpata mgombea wa nafasi hiyo kupitia chama chake cha Republican kupitia mkutano mkuu wa chama chake mjini Cleveland.

10-donald-trump-debate.w750.h560.2x

Baada ya kuchaguliwa kuwa mgombea urais Donald Trump alitoa shukran zake kupitia mtandao wa twitter, na imetanabahishwa kwamba gavana wa jimbo la Indiana Mike Pence, ndiye mgombea mwenza .

Taarifa zaidi zinasema watoto wawili wa Donald Trump wa kiume Donald na pia bintiye Tiffany wanatarajiwa kuhutubia mkutano mkuu wa wanachama wa chama hicho.

Leave A Reply